Proverbs 1:25-31

25 akwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote
na hamkukubali karipio langu,
26 bmimi nami nitawacheka katika maafa yenu,
nitawadhihaki wakati janga litawapata:
27 cwakati janga litawapata kama tufani,
wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli,
wakati dhiki na taabu zitawalemea.

28 d“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu;
watanitafuta lakini hawatanipata.
29 eKwa kuwa walichukia maarifa,
wala hawakuchagua kumcha Bwana,
30 fkwa kuwa hawakukubali mashauri yangu,
na kukataa maonyo yangu,
31 gwatakula matunda ya njia zao,
na watashibishwa matunda ya hila zao.
Copyright information for SwhNEN